Droo ya hatua ya robo fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho la CRDB (FA) imefanyika leo ambapo mabingwa watetezi Yanga wamepangwa kuchuana na Stand United
Endapo Yanga itavuka hatua ya robo fainali, mechi ya nusu fainali itacheza na mshindi wa mchezo kati ya JKT Tanzania dhidi ya Pamba Jiji
Nao Wekundu wa Msimbazi, Simba wataumana na Mbeya City katika mchezo wa kuwania tiketi ya kutinga nusu fainali
Endapo Simba itavuka kizingiti cha Mbeya City na kutinga nusu fanali, katika hatua hiyo itachuana na mshindi wa mchezo kati ya Singida BS dhidi ya Kagera Sugar




