Timu ya Ngorongoro Heroes inatarajia kuingia kambini Jumatano, Aprili 9, 2025 kwaajili ya maandalizi ya mashindano ya Afcon U20 itakayopigwa Misri kuanzia Aprili 27 huku fainali ikitarajiwa kuchezwa May 18
Ngorongoro ilikata tiketi ya kushiriki michuano hiyo baada ya kutwaa ubingwa CECAFA 2024 kwa kuipiga Kenya mabao 2-1 kwenye mchezo wa fainali uliochezwa katika Uwanja wa KMC Complex jijini Dar es Salaam
Ngorongoro itakwenda kupambana na timu nyingine 11 ambazo ni Morocco, Misri, Senegal, Siera leone, Ghana, Nigeria, DR Congo, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Kenya, Tanzania, Zambia na Afrika kusini



