Local,Transfer News,Yanga, Azam

Yanga yapania kumrejesha Fei Toto

Joel JJ By Joel JJ
β€’
16 Apr 2025
Yanga yapania kumrejesha Fei Toto

Katika dirisha lijalo la usajili linalotarajiwa kuwa na vuguvugu kubwa, klabu ya Yanga SC imehusishwa na mipango ya kumsajili tena kiungo mshambuliaji mahiri, Feisal Salum, maarufu kama "Fei Toto", ambaye kwa sasa anakipiga katika klabu ya Azam FC.

Feisal alijiunga na Azam FC misimu miwili iliyopita akitokea Yanga SC, katika uhamisho uliotawaliwa na sintofahamu na mgogoro mkali baina yake na klabu hiyo ya Jangwani

Tofauti hizo zilileta mgawanyiko mkubwa miongoni mwa mashabiki na wadau wa soka nchini, huku kila upande ukitoa kauli zenye hisia kali juu ya uamuzi huo.

Hata hivyo, hali imeonekana kubadilika kwa sasa, huku tetesi zikiendelea kuvuma kuwa Yanga SC wanapanga kumrudisha nyota huyo kwa ajili ya kuimarisha kikosi chao kuelekea msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara na michuano ya kimataifa

Chanzo cha karibu na uongozi wa klabu hiyo kimeeleza kuwa mazungumzo ya awali tayari yameanza na kuna uwezekano mkubwa dili hilo likakamilika mwez Juni

Feisal Salum amekuwa na mchango mkubwa katika mafanikio ya Azam FC tangu alipojiunga nao, akionyesha kiwango bora, maarifa ya hali ya juu uwanjani, na uwezo wa kuamua mechi.

Umahiri wake katika eneo la kiungo cha ushambuliaji, pasi za mwisho na mabao ya mbali umemfanya kuwa mmoja wa wachezaji wanaohitajika mno nchini.

Iwapo atarejea Jangwani, Feisal atakuwa anajiunga na kikosi kilichoimarika zaidi na ambacho kinatafuta mafanikio ya ndani na nje ya nchi. Hii pia itakuwa fursa ya yeye kuandika ukurasa mpya wa historia yake na Yanga, baada ya kuondoka kwa hali ya mvutano miaka miwili iliyopita.

Mashabiki wengi wa Yanga tayari wameanza kuonyesha matumaini na hamasa kuhusu uwezekano wa kurejea kwa fundi huyo, huku wengine wakisubiri kwa tahadhari kuona iwapo uongozi wa klabu utaweza kufanikisha dili hilo.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
7m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
36m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’