Kamwe, Mazanzala wakumbana na rungu la TFF

Joel JJ By Joel JJ β€’ 19th April 2025


Kamwe, Mazanzala wakumbana na rungu la TFF

Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ilikutana kwa ajili ya kupitia na kutoa uamuzi wa mashauri yaliyowasilishwa mbele yake

Miongoni mwa mashauri hayo yaliwahusu wasemaji wa vilabu vya Yanga, Simba na Kagera Sugar ambao ni Ali Kamwe, Ahmed Ali na Hamis Mazanzala ambao walituhumiwa kwa makosa ya kuchochea UMMA

Katika maamuzi yake, Kamati imewatia hatiani Kamwe, na Mazanzala na kuwapa adhabu ya kulipa faini ya Tsh Milioni 5 pamoja na onyo la kutofanya kosa la kimaadili ndani ya kipindi cha miaka miwili

Upande wa msemaji wa Simba Ahmed Ali yeye amenusurika na adhabu hiyo baada ya kutopatikana na hatia

Lakini adhabu kama hiyo imemkumba mwanachama wa Simba Mohammed Khamis Mohammed ambaye pia alifikishwa mbele ya Kamati kutokana na makosa ya uchochezi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.