Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ilikutana kwa ajili ya kupitia na kutoa uamuzi wa mashauri yaliyowasilishwa mbele yake
Miongoni mwa mashauri hayo yaliwahusu wasemaji wa vilabu vya Yanga, Simba na Kagera Sugar ambao ni Ali Kamwe, Ahmed Ali na Hamis Mazanzala ambao walituhumiwa kwa makosa ya kuchochea UMMA
Katika maamuzi yake, Kamati imewatia hatiani Kamwe, na Mazanzala na kuwapa adhabu ya kulipa faini ya Tsh Milioni 5 pamoja na onyo la kutofanya kosa la kimaadili ndani ya kipindi cha miaka miwili
Upande wa msemaji wa Simba Ahmed Ali yeye amenusurika na adhabu hiyo baada ya kutopatikana na hatia
Lakini adhabu kama hiyo imemkumba mwanachama wa Simba Mohammed Khamis Mohammed ambaye pia alifikishwa mbele ya Kamati kutokana na makosa ya uchochezi



