Msimu wa pili wa ligi ya Muungano unazinduliwa rasmi leo kule Gombani, Pemba kwa mechi ya kwanza ya robo fainali kupigwa
Singida Black Stars itazindua pazia la michuano hiyo kwa kumenyana na wenyeji JKU katika mchezo utakaopigwa saa 11 jioni
Mshindi wa mchezo huo atatinga nusu fainali na kumsubiri mshindi wa robo fainali ya tatu kati ya KMKM dhidi ya Azam Fc, mchezo utakaopigwa kesho Ijumaa, saa 1:15 usiku
Mapema Ijumaa, mechi ya robo fainali ya pili itapigwa kati ya Zimamoto dhidi ya Coastal Union, mchezo utakaopigwa saa 10 jioni
Mshindi wa robo fainali ya pili, atachuana na mshindi wa robo fainali ya nne kati ya KVZ dhidi ya Yanga mchezo utakaopigwa Jumamosi, saa 1:15 usiku
Mechi za nusu fainali zitapigwa April 28 na April 29 wakati mchezo wa fainali utapigwa May 1, 2025



