International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu, April 28 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Apr 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu, April 28 2025

Atletico Madrid wameweka beki wa Tottenham raia wa Argentina, Cristian Romero, 27, kama moja ya wachezaji itakaowasajili msimu huu wa joto. (Marca)

Manchester City wanatarajiwa kumsajili beki wa pembeni wa Juventus na Italia, Andrea Cambiaso, 25, huku klabu hiyo ya Italia ikielekeza macho yake kwa beki wa Arsenal raia wa Ureno, Nuno Tavares, 25, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Lazio. (Sun)

Newcastle United, Manchester United, Tottenham, West Ham, Chelsea na Liverpool zote zinamwania mshambuliaji wa Canada Jonathan David, 25, ambaye mkataba wake na Lille unamalizika msimu wa joto, lakini Marseille wanajaribu kumshawishi aendelee kubaki Ufaransa. (RMC sports)

Manchester United wamempa mshambuliaji wa Wolves, Matheus Cunha, mkataba wa miaka mitano iwapo Mbrazi huyo mwenye umri wa miaka 25 ataamua kuhamia Old Trafford. (Teamtalk)

Chelsea wanajitahidi kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa Juventus, Kenan Yildiz, 19, lakini wanakutana na ushindani kutoka Arsenal, Liverpool, Manchester United na Manchester City wanaomtaka pia mchezaji huyo wa kimataifa wa Uturuki. (Caught Offside)

Manchester United bado wana nia ya kumsajili mshambuliaji wa Crystal Palace raia wa Ufaransa, Jean-Philippe Mateta, 27, iwapo watashindwa kumchukua mshambuliaji wa Ipswich Town raia wa Uingereza, Liam Delap, 22. (GiveMeSport)

Newcastle United wanafanyia kazi dili la kumsajili beki wa kimataifa wa Korea Kusini, Kim Min-jae, 28, kutoka Bayern Munich msimu huu wa joto. (Football Insider)

Orodha ya Newcastle ya wachezaji inaowataka kuimarisha safu yao ya ulinzi pia inajumuisha Ousmane Diomande wa Sporting, mwenye umri wa miaka 21 kutoka Ivory Coast, Malick Thiaw wa AC Milan, beki wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 23, na Jan Paul van Hecke, 24, kutoka Brighton. (GiveMeSport)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’