Arsenal wanafikira kumsajili mshambuliaji wa Chelsea na Ufaransa Christopher Nkunku, 27, ambaye hayuko katika mipango ya timu ya Chelsea kwa sasa, huku Mikel Arteta akitafuta kuongeza nguvu katika safu ya ushambuliaji msimu huu wa kiangazi. (Teamtalk)
DC United wamekuwa kwenye mazungumzo ya mkataba kwa miezi kadhaa na kiungo wa zamani wa Manchester United, Juventus na Ufaransa Paul Pogba, 32, ambaye hajacheza soka kwa miezi 20. (Washington Post)
Mabingwa wa Ligi Kuu England Liverpool wanatarajia kuwekeza kiasi kikubwa kwenye kikosi chao msimu huu wa kiangazi, huku mshambuliaji wa kati na beki wa kushoto wakiwa kipaumbele chao cha kwanza. (Telegraph)
Chelsea wanapanga kumsajili winga wa Borussia Dortmund Jamie Gittens, 20, raia wa Uingereza, kabla ya Kombe la Dunia la Klabu, na kuna uwezekano wakamuuza mshambuliaji wa England Jadon Sancho, 25, kwa klabu hiyo ya Ujerumani kama sehemu ya mpango huo.
Sancho kwa sasa yuko kwa mkopo Stamford Bridge kutoka Manchester United, lakini Chelsea wana wajibu wa kufanya mkataba huo kuwa wa kudumu. (Teamtalk)
Rais wa Real Sociedad Jokin Aperribay amesema mustakabali wa kiungo wa kati wa Hispania Martin Zubimendi, 26, ambaye anasakwa na Arsenal, utaamuliwa mwezi Juni. The Gunners wako tayari kuanzisha mchakato wa kulipa pauni milioni 51. (Radio Marca Donostia)
Everton wamemweka mshambuliaji wa Tottenham Hotspur na Brazil Richarlison, 27, kama kipaumbele chao kikuu msimu huu wa kiangazi. (Givemesport)
Kiungo wa Newcastle raia wa Uingereza Sean Longstaff, 27, anasakwa na Leeds United. (i Paper)
Spurs italazimika kuuza wachezaji ili kupata fedha kwa ajili ya usajili mpya msimu huu wa kiangazi. (Telegraph) Mwenyekiti wa Leeds Paraag Marathe anasafiri kwenda Uingereza kufanya mazungumzo kuhusu mustakabali wa kocha Daniel Farke. (Guardian)
Fulham wanavutiwa kumsajili beki wa kulia wa England Kyle Walker-Peters, 28, kwa uhamisho wa bure pindi mkataba wake na Southampton utakapoisha msimu huu wa kiangazi. (Sky Sports)
Arsenal wako tayari kuanza mazungumzo na wakala wa mshambuliaji wa Sporting na Sweden Viktor Gyokeres, 26, kuhusu uhamisho msimu huu wa kiangazi. (Givemesport)
Real Betis huenda ikashindwa kufikia bei ya Manchester United kwa ajili ya winga wa Brazil Antony licha ya klabu hiyo ya La Liga kuonyesha nia ya kufanya mkopo wake kuwa uhamisho wa kudumu. (Mirror)
Manchester United bado wanavutiwa kumsajili mshambuliaji wa Napoli na Nigeria Victor Osimhen, 26, lakini kuna wasiwasi kuhusu mpango huo Old Trafford. (TBF Football)
Everton wako kwenye mazungumzo na kiungo wa Senegal Idrissa Gueye, 35, kuhusu mkataba mpya. (Football Insider)
Wrexham, Bolton, Charlton na Portsmouth wanavutiwa na mshambuliaji wa Dungannon Swifts kutoka Ireland ya Kaskazini Tomas Galvin, 20. (Football League World)
BBC



