Mlinda lango Aboutwalib Mshery ameibuka shujaa kwenye mikwaju ya penati akiokoa mikwaju miwili muhimu na kuipeleka Yanga fainali ya kombe la Muungano baada ya ushindi wa penati 3-1 dhidi ya Zimamoto
Dakika 90 za mchezo huo zilimalizika kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 Yanga ikitangulia kufunga bao lake kwenye kipindi cha kwanza kupitia Maxi Nzengeli





