Licha ya Yanga kugomea mchezo namba 184 dhidi ya Simba uliohirishwa March 08, Bodi ya Ligi (TPLB) leo imekata mzizi wa fitina kwa kuupangia tarehe mchezo huo
Kulingana na maboresho ya ratiba yaliyotolewa TPLB mapema leo, mchezo huo sasa utapigwa Juni 15
Aidha mechi mbili kuhitimisha msimu sasa zitapigwa Juni 18 na Juni 22 ambapo zote zitachezwa katika muda mmoja ili kuepuka upangaji wa matokeo




