International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne May 06 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
6 May 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne May 06 2025

Manchester United imeiambia Chelsea kwamba italazimika kulipa pauni milioni 65 ili kumsajili winga wa Argentina mwenye umri wa miaka 20 Alejandro Garnacho msimu huu wa kiangazi. (Star)

Klabu za Everton na Wolves zina nia ya kumsajili mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Nicolas Pepe, huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 29 akitarajiwa kukamilisha mkataba wake na klabu ya Villarreal msimu wa kiangazi. (Foot Mercato - in French)

Winga wa Ujerumani Leroy Sane, 29, amebadilisha wakala wake, jambo ambalo limeibua swali kuhusu mustakabali wake katika klabu ya Bayern Munich na kuongeza mkataba ambao ulikaribia kuafikiwa. (Sky Sports in Germanty)

Beki wa Liverpool anayeondoka Trent Alexander-Arnold yuko tayari kusaini mkataba wa miaka sita na Real Madrid ambao utaanza kutekelezwa Julai mosi. (Atheletic- Usajili unahitajika)

Alexander-Arnold, 26, alikataa ofa ya nyongeza ya mshahara ili kusalia na Liverpool hadi mwisho wa msimu huu. (ESPN)

Liverpool inatazamiwa kutumia fedha nyingi msimu huu wa kiangazi huku Reds wakiwa mbioni kuwasaka mabeki wapya wa safu ya kushoto na kati pamoja na mshambuliaji. (Sport)

Chelsea inatarajiwa kufanya mazungumzo na kiungo wa Ecuador Moises Caicedo, 23, kuhusu kandarasi mpya msimu huu kama zawadi kwa uchezaji wake mzuri msimu huu. (Telegraph - usajili unahitajika)

Mlinda lango wa Southampton na England Aaron Ramsdale, 26, anawaniwa na klabu za Manchester United na West Ham. (Mirror)

Aston Villa inamfuatilia mlinda lango wa Real Madrid na Ukraine Andriy Lunin, 26, huku mlinda lango wa Argentina Emiliano Martinez, 32, akiendelea kuhusishwa na tetesi za uhamisho wa majira ya kiangazi. (Birmingham Mail)

Meneja wa Fulham Marco Silva na mkufunzi wa Nottingham Forest Nuno Espirito Santo ni miongoni mwa wagombea wanaowaniwa na klabu ya Saudi Pro League Al-Hilal. (Sport )

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’