Kikosi cha Simba kitaondoka jijini Dar es salaam leo Jumanne, May 13 kuelekea Morocco tayari kwa mchezo wa mkondo wa kwanza fainali ya kombe la Shirikisho (CAF CC) dhidi ya RS Berkane
Mchezo huo utapigwa Jumamosi, May 17 katika uwanja wa Manispaa ya Berkane, saa 4 usiku kwa saa za Tanzania
Msafara wa Simba ambao utajumuisha wachezaji, benchi la ufundi, viongozi na mashabiki utaondoka saa 3 usiku kwa kutumia usafiri wa ndege y ATCL iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dk. Samia Suluhu Hassan
Itakuwa itakuwa safari ya takribani saa 7 hadi jiji la Casablanca ambapo kikosi kitatua jijini humo Alfajiri ya Jumatano, May 14
Simba inakwenda Morocco ikiwa na dhamira ya kusaka matokeo mazuri ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kutwaa taji la Shirikisho katika mchezo wa mkondo wa pili utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa, May 25



