International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi May 15 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
15 May 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi May 15 2025

Manchester City wamekutana na mshambuliaji wa Bayer Leverkusen Florian Wirtz, 22, kuhusu uhamisho katika majira ya joto. (Bild)

Hata hivyo, Liverpool pia wamewasiliana na Wirtz kuonyesha nia ya kumsajili kiungo huyo mshambuliaji katika majira haya ya joto. (Athletic)

Klabu za Ligi Kuu ya England zikiwemo Manchester City na Arsenal zinamnyatia mshambuliaji wa Real Madrid Rodrygo, 24, kufuatia ripoti za Mbrazil huyo kutoelewana na baadhi ya wafanyakazi wa klabu. (AS)

Real Madrid wako tayari kulipa pauni milioni 50 kumnunua beki wa kati wa Kihispania Dean Huijsen, 20, kutoka Bournemouth. (Sky Sports)

Mshambuliaji wa Manchester United Joshua Zirkzee, 23, anasakwa na Inter Milan katika majira ya joto baada ya kiwango kibovu alichooshesha Mholanzi huyo msimu huu. (Corriere dello Sport)

Liverpool hawatakubali ada ya pauni 850,000 kutoka Real Madrid kumruhusu beki Trent Alexander-Arnold, 26, kuhamia klabu hiyo ya Uhispania mapema ili acheze michuano ya kombe la dunia kwa vilabu. (Sun)

Newcastle wamewapita Chelsea katika kinyang'anyiro cha kumsajili beki wa Kiingereza Marc Guehi, 24, kutoka Crystal Palace. (Teamtalk)

Bayern Munich wamekubaliana ada na Bayer Leverkusen kumsajili beki wa kati wa Ujerumani Jonathan Tah, 29. (Fabrizio Romano)

Barcelona wana nia ya kushindana na Arsenal katika kumsajili kipa wa Espanyol Joan Garcia, 24. (AS)

Barcelona wako tayari kuwaondoa hadi wachezaji nane wa kikosi cha kwanza katika majira haya ya joto ili kupata fedha za kusajili wachezaji wapya na kuboresha mikataba ya waliopo. (Mirror)

Barca wanataka kumsajili beki wa kati, beki wa pembeni na winga wa kumsaidia nyota wa Hispania mwenye umri wa miaka 17 Lamine Yamal. (Espn)

Xavi Simons wa RB Leipzig yuko tayari kuondoka klabuni hapo katika majira haya ya joto, licha ya kiungo huyo Mholanzi mwenye umri wa miaka 22 kusaini mkataba wa kudumu mwezi Januari. (Fabrizio Romano)

Bristol City wanataka kumbakisha mshambuliaji Nahki Wells, 34, msimu ujao baada ya kushindwa kufuzu kwa Ligi Kuu kupitia mchujo wa Championship. (Sky Sports)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’