Fanali ya kwanza ya kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF CC) imemalizika RS Berkane wakitumia vyema uwanja wa nyumbani kwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0
Dakika 15 za kwanza ndizo zilizovuruga hesabu za Simba katika mchezo huo wakiruhusu mabao mawili mepesi yakitokana na kukosekana umakini katika ulinzi
Hata hivyo baada ya kuingia mabao hayo Simba ilirejea mchezoni na unaweza kusema kipindi cha pili Simba ilikuwa bora zaidi lakini changamoto ilikuwa katika matumizi ya nafasi
Sio matokeo mazuri kwa Simba lakini pia sio matokeo mabaya sana, kwani Simba itahitaji kufunga angalau mabao mawili katika mchezo wa marudiano utakaopigwa wiki ijayo visiwani Zanzibar ili kulazimisha mchezo huo kwenda kwenye matuta
Ushindi wa mabao 3-0 utatosha kuipa Simba ubingwa wa michuano hiyo kwa mara ya kwanza katika historia yake



