Yanga imetinga fainali ya kombe la CRDB ikiichapa JKT Tanzania mabao 2-0 katika mchezo wa nusu fainali uliopigwa uwanja wa Mkwakwani
Mabao ya Prince Dube na Mudathir Yahya aliyefunga bao la pili dakika za jiooooni, aliihakikishia Yanga kutinga fainali ya tano mfululizo ya michuano hiyo
Pengine ni mchezo ambao mabao mawili yalionekana machache kwa Yanga nafasi za wazi nyingi hazikubadilishwa mabao na Stephane Aziz Ki na Maxi Nzengeli ambao pengine leo kila mmoja angeweza kuondoka na mpira
Ilikuwa mechi ngumu iliyochangiwa na mazingira ya dimba la Mkwakwani lililoja maji kutokana na mvua kubwa iliyonyesha mapema mkoani Tanga



