Simba yaja na mikakati mipya ya kuikabili Berkane Zanzibar

Joel JJ By Joel JJ β€’ 20th May 2025


Simba yaja na mikakati mipya ya kuikabili Berkane Zanzibar

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ali amesema baada ya jitihada za kurejesha mchezo wa mkondo wa pili fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF CC) dhidi ya RS Berkane katika uwanja wa Benjamin Mkapa kukwama, hakuna tena muda wa kulalamika na sasa Simba inakwenda kujiandaa na mchezo huo utakaopigwa Jumapili, May 25 katika uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar

Akizungumza katika Mkutano na wanahabari uliofanyika Makao Makuu ya Simba, Osterbay jijini Dar es salaam, Ahmed alisema Simba ilipambana mchezo huo upigwe uwanja wa Benjamin Mkapa ili kuwapunguzia gharama mashabiki wao ambao wengine wanasafiri kutoka mikoani

"Tuna mashabiki wamekata tiketi kutoka mikoa ya mbali, tathmni yetu ilionyesha pengine watahitaji kuwa na sio chini ya laki tatu kuweza kufika Zanzibar kushuhudia mchezo huo na kisha kurejea makwao"

"Lakini pia uwanja wa Benjamin Mkapa ungetoa nafasi ya mashabiki wengi zaidi kushuhudia mchezo huo wa kihistoria kwani watu 60,000 wangeingia uwanjani"

"Kwa kuwa jitihada zetu zimekwama, basi hatuna sababu ya kuendelea kulalamika. Lengo letu ya kutwaa ubingwa Afrika liko palepale kwa hiyo tunapaswa kuanza maandalizi ya mchezo dhidi ya Berkane utakaopigwa Jumapili, May 25 katika uwanja wa New Amaan Complex, saa 10 jioni," alisema Ahmed

Ahmed amebainisha kuwa Kikosi cha Simba kitasafiri kesho Jumatano kwenda Zanzibar kwaajili ya kuanza maandalizi ya mchezo huo

Ahmed amesema kwa mashabiki ambao walikata tiketi kushuhudia mchezo huo katika uwanja wa Benjamin Mkapa, watazitumia tiketi hizo katika Tamasha la Simba Day litakalofanyika baadae mwaka huu katika kuukaribisha msimu wa mashindano 2025/26

Utaratibu mpya wa viingilio umetangazwa ambapo viingilio vipya ni VIP 50,000/- URUSI 30,000/- na Mzunguuko 10,000/-


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.