Mlinzi wa kulia wa Yanga Yao Kouassi 'Jeshi' amefanyiwa upasuaji wa goti nchini Morocco
Yao amekuwa nje ya uwanja kwa takribani miezi minne sasa akisumbuliwa na maaumivu ya goti
Nyota huyo raia wa Ivory Coast, anatarajiwa kuwa nje ya uwanja hadi miezi sita. Huenda klabu ya Yanga ikalazimika kurudi sokoni kusaka mbadala wake
Mkataba wake na mabingwa hao wa Tanzania, unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu





