Berkane yatwaa kombe la Shirikisho (CAF CC)

Joel JJ By Joel JJ β€’ 25th May 2025


Berkane yatwaa kombe la Shirikisho (CAF CC)

Simba imekosa kombe la Shirikisho (CAF CC) baada ya kulazimiswa sare ya bao 1-1 dhidi ya RS Berkane katkika mchezo wa pili wa fainali uliopigwa uwanja wa New Amaan Complex

Kulikuwa na kila dalili kwa Simba kupindua meza leo baada ya kufunga bao la mapema dakika ya 17 kupitia kwa Joshua Mutale ambaye leo alikuwa nyota wa mchezo

Kazi nzuri ya Steven Mukwala kutoka winga ya kulia krosi yake ya chinichini iliwapita walinzi wa Berkane na kumkuta Mutale

Simba iliendelea kutawala mchezo na kipindi cha pili Steven Mukwala akafunga bao akiujaza kambani mpira wa adhabu uliopigwa Jean Charles Ahoua

Hata hivyo VAR ilifuta bao hilo katika mazingira tatanishi Mukwala akidaiwa kuwa ameotea

Berkane walifunga bao la kusawazisha dakika za lala salama kupitia shambulizi la kushitukiza

Lakini unaweza kusema kadi nyekundu aliyopewa Yusuph Kagoma mapema katika kipindi cha pili ndio iliyovuruga mipango ya Simba katika mchezo huo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.