Simba imekosa kombe la Shirikisho (CAF CC) baada ya kulazimiswa sare ya bao 1-1 dhidi ya RS Berkane katkika mchezo wa pili wa fainali uliopigwa uwanja wa New Amaan Complex
Kulikuwa na kila dalili kwa Simba kupindua meza leo baada ya kufunga bao la mapema dakika ya 17 kupitia kwa Joshua Mutale ambaye leo alikuwa nyota wa mchezo
Kazi nzuri ya Steven Mukwala kutoka winga ya kulia krosi yake ya chinichini iliwapita walinzi wa Berkane na kumkuta Mutale
Simba iliendelea kutawala mchezo na kipindi cha pili Steven Mukwala akafunga bao akiujaza kambani mpira wa adhabu uliopigwa Jean Charles Ahoua
Hata hivyo VAR ilifuta bao hilo katika mazingira tatanishi Mukwala akidaiwa kuwa ameotea
Berkane walifunga bao la kusawazisha dakika za lala salama kupitia shambulizi la kushitukiza
Lakini unaweza kusema kadi nyekundu aliyopewa Yusuph Kagoma mapema katika kipindi cha pili ndio iliyovuruga mipango ya Simba katika mchezo huo



