International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano May 28 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 May 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano May 28 2025

Klabu ya Saudi Pro League, Al-Hilal, imempa nahodha wa Manchester United, Bruno Fernandes, 30, ofa ya mkataba na kumwambia kiungo huyo wa Ureno ana saa 72 kufanya uamuzi. (Mail)

Manchester City wameingia katika mbio za kumsajili kiungo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 21 wa Lyon, Rayan Cherki, ambaye pia amehusishwa na vilavu vya Liverpool na Chelsea. (Telegraph)

Tottenham wamepewa fursa ya kumsajili winga wa Bayern Munich na Ujerumani, Leroy Sane, 29, ambaye atakuwa huru mwishoni mwa mwezi ujao. (Sky Sports)

Everton wamejiunga na Leeds United katika mbio za kumsajili mshambuliaji wa Newcastle United na England mwenye umri wa miaka 33, Callum Wilson, ambaye mkataba wake unamalizika mwezi ujao. (The Sun)

Manchester United wamekubali mpango wa malipo ya Liam Delap kwa Ipswich Town na sasa wanasubiri mshambuliaji huyo wa England kuamua hatua yake inayofuata. (ESPN)

Mshambuliaji wa Ureno, Cristiano Ronaldo, 40, anatarajiwa kuondoka Al-Nassr ya Saudi Pro League na kusaini mkataba na klabu mpya kucheza Kombe la dunia la klabu, ambalo litaanza Juni 15 nchini Marekani. (Telegraph)

Aston Villa wanaonekana kuwa tayari kumsajili mshambuliaji wa Uholanzi mwenye umri wa miaka 18 wa Feyenoord, Zepiqueno Redmond, kwa uhamisho huru msimu huu wa joto. (Sky Sports)

Arsenal wamefanya mazungumzo na wakala wa mshambuliaji wa Sporting, Viktor Gyokeres, huko Lisbon na kutoa ofa ya pauni milioni 58.7 kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Sweden. (Correio da Manha)

BBC

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
3m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
32m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’