Local,Transfer News,Yanga, Zamalek

Zamalek yakaribia kumnasa Mzize

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 May 2025
Zamalek yakaribia kumnasa Mzize

Klabu ya Zamalek ya Misri imeongeza kasi ya harakati zake za kumsajili mshambuliaji tegemeo wa Yanga SC, Clement Mzize, kwa kuongeza dau lao la awali ambalo lilikataliwa na mabosi wa klabu hiyo ya Tanzania.

Kwa mujibu wa vyanzo vya karibu na uongozi wa Yanga, Zamalek tayari imetuma ofa mpya ya takribani dola 750,000 za Kimarekani, sawa na zaidi ya shilingi bilioni 2 za Kitanzania, ikiwa ni jitihada mpya ya kuhakikisha wanamnasa Mzize kabla ya dirisha la usajili kufungwa.

Awali, Yanga ilipokea ofa ya chini kutoka kwa Zamalek, lakini ilikataliwa kwa kuwa haikufikia matarajio ya klabu hiyo ambayo ipo kwenye harakati za kutetea ubingwa wake wa Ligi Kuu na kombe la CRDB. Hata hivyo, ongezeko la dau limefungua milango ya mazungumzo ya moja kwa moja kati ya pande hizo mbili.

Mbali na Zamalek, inadaiwa kuwa Yanga pia imepokea ofa kutoka klabu ya JS Kabylie ya Algeria na Al-Ittihad ya Libya, lakini hakuna hata moja iliyofanikiwa kuwashawishi viongozi wa Yanga kama ilivyofanya Zamalek.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, kuna kila dalili kwamba Mzize atatua Zamalek, huku usajili wake ukitarajiwa kuiingizia Yanga kitita kizito cha fedha ambacho kitasaidia katika mipango ya maboresho ya kikosi chao.

Ni dhahiri kuwa Yanga imeanza kuingia sokoni kufanya biashara ya wachezaji wake nyota, jambo lililoonekana wazi baada ya kumuuza kiungo wake nyota Stephane Aziz Ki kwa Wydad Athletic ya Morocco kwa ada ya karibu Tsh Bilioni 2.

Mlinda mlango namba moja wa timu hiyo, Djigui Diarra, naye anatajwa kuwa katika rada za klabu mbalimbali, huku taarifa zikieleza kuwa Yanga imepokea ofa za kuvutia kutoka nje ya nchi.

Yanga inaonekana kuwa katika mpango wa kuongeza mapato kupitia mauzo ya baadhi ya wachezaji, huku ikijiandaa kufanya usajili wa maboresho kuelekea msimu ujao wa mashindano ya ndani na kimataifa.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
44m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’