Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano Juni 04 2025

Joel JJ By Joel JJ β€’ 4th June 2025


Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano Juni 04 2025

Mshambuliaji wa Tottenham Son Heung-min analengwa na vilabu vya Saudi Arabia na Spurs wanaweza kuchagua kumnunua Mkorea Kusini mwenye umri wa miaka 32 huku wakitafuta pesa za uhamisho. (Telegraph)

Kiungo wa kati wa Real Sociedad Martin Zubimendi, 26, ametia shaka juu ya kuhamia Arsenal, huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania akisema ana "chaguo" na hana uhakika ni wapi ataishia. (Redio Nacional de Espana, via Metro)

Winga wa Manchester United Jadon Sancho pia anaweza kuelekea Saudi Pro League huku Al-Hilal , Al-Ittihad na Al-Nassr wote wakimtaka mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza mwenye umri wa miaka 25. (Mirror)

Mshambuliaji wa Brentford na Cameroon Bryan Mbeumo, 25, anatumai mshahara wa pauni 250,000 kwa wiki - mara tano ya mshahara wake wa sasa - ikiwa atajiunga na Manchester United . (Time - subcription require)

Inter Milan wamefanya mawasiliano na meneja wa Como Cesc Fabregas kuhusu kiungo huyo wa zamani wa Uhispania kuchukua nafasi ya meneja wao mpya baada ya kuondoka kwa Simone Inzaghi. (Sky Sports Italia - in Italian)

Kiungo wa kati wa Croatia Luka Modric, 39, amekubali kwa kauli yake kujiunga na AC Milan atakapoondoka Real Madrid baada ya Kombe la Dunia la Vilabu la Fifa msimu huu wa joto. (Gianluca di Marzio, via Football Italia)

Mmiliki wa sehemu wa Crystal Palace John Textor, ambaye pia anamiliki klabu ya Ufaransa ya Lyon , anajaribu kuuza sehemu yake kubwa katika klabu hiyo huku The Eagles wakijaribu kuepuka kuondolewa kwenye Ligi ya Ulaya msimu ujao kwa kuvunja sheria za Uefa za umiliki wa vilabu vingi. (Mirror)

Mlindalango wa Uingereza Aaron Ramsdale amefanya mazungumzo kuhusu kuhamia West Ham kutoka Southampton, ambao wanatarajia kupata pauni milioni 20 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 kufuatia klabu hiyo kushuka daraja kutoka Ligi ya Premia. (Sport)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.