Klabu ya Azam Fc imekamilisha usajili wa mlinda lango wa Simba Aishi Manula kwa mkataba wa miaka miwili
Manula anakamilisha mkataba wake na Simba mwishoni mwa mwezi hivyo anajiunga na Azam Fc akiwa mchezaji huru
Kurejea Azam Fc kwa Manula ni kama amerejea nyumbani kwani Simba ilimsajili mwaka 2017 akitokea klabu hiyo
Manula ameitumikia Simba kwa takribani misimu nane akiwa kipa tegemeo kwa misimu sita mfululizo
Wanasimba watamkumbuka Manula kwa utumishi wake katika kipindi hicho licha ya kuwa hapa mwishoni aliingia katika mgogoro wa 'chinichini' na viongozi wa Simba baada ya tuhuma za kuhujumu katika mchezo dhidi ya Yanga msimu uliopita



