Mtendaji Mkuu wa Yanga Andre Mtine leo ameitikia wito wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuhakiki madeni pamoja na madai ya Yanga kulipwa fedha za ubingwa wa kombe la FA (CRDB)
Yanga imekuwa na malimbikizo ya madai ya zawadi ya ubingwa wa michuano hiyo kwa misimu mitatu
Mtine ameeleza msimamo wa Yanga ni kulipwa fedha hizo kwani wanahitaji kufanya maandalizi kuelea mchezo wa fainali, bila ya kulipwa hawawezi kuiandaa timu kwa ajili ya mchezo huo
"Tumefika hapa wakatuelekeza kwenda kuzungumza na wahasibu wao, tumewaeleza msimamo wetu, tunataka watulipe fedha zetu ili tuweze kuiandaa timu kwa ajili ya mchezo wa fainali"
"Masuala ya mahesabu ya madeni na mapato yatafanyika katika msimu husika, huwezi kuzuia pesa tunayostahili msimu huu kwa kusubiri madeni ya msimu ujao, mmesikia kitu kama hiki kikifanyika wapi?"
"Kama wana jambo lolote wanapaswa kututaarifu kwa maandishi, hatuwezi kuendeleza majibizano mitandaoni kwa sasa," alisema Mtine
Yanga imeendelea kushikilia msimamo wake wa kutocheza fainali dhidi ya Singida Black Stars Juni 28 kama haitalipwa fedha hizo



