Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' imehitimisha safari yake katika michuano ya COSAFA kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Eswatini mabao ya Stars ykifungwa na Iddi Nado na Shekhan Khamis
Tanzania imemaliza katika nafasi ya pili kwenye Kundi C nyuma ya vinara Madagascar (Pointi 4) na mbele ya Eswatin (Pointi 1)
Kabla ya mechi mbili za COSAFA, Stars ilicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Afrika Kusini ikilazimishwa suluhu ya bila kufungana
Ilipoteza mechi ya kwanza katika michuano ya COSAFA kwa kufungwa bao 1-0 na Madagascar



