Stars yahitimisha COSAFA kwa ushindi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 11th June 2025


Stars yahitimisha COSAFA kwa ushindi

Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' imehitimisha safari yake katika michuano ya COSAFA kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Eswatini mabao ya Stars ykifungwa na Iddi Nado na Shekhan Khamis

Tanzania imemaliza katika nafasi ya pili kwenye Kundi C nyuma ya vinara Madagascar (Pointi 4) na mbele ya Eswatin (Pointi 1)

Kabla ya mechi mbili za COSAFA, Stars ilicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Afrika Kusini ikilazimishwa suluhu ya bila kufungana

Ilipoteza mechi ya kwanza katika michuano ya COSAFA kwa kufungwa bao 1-0 na Madagascar


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.