Bodi ya ligi yamaliza utata waamuzi wa dabi ya Kariakoo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd June 2025


Bodi ya ligi yamaliza utata waamuzi wa dabi ya Kariakoo

Bodi ya Ligi (TPLB) imewatangaza waamuzi wa mchezo wa Dabi ya Kariakoo kati ya Yanga dhidi ya Simba utakaopigwa Jumatano, Juni 25 katika uwanja wa Benjamin Mkapa ambapo waamuzi wote wanatoka nchini Misri

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Bodi mapema leo, mchezo huo namba 184 utaamuliwa na waamuzi kutoka Misri ambapo Mwamuzi wa kati ni Amin Mohamed Amin Omar (Misri), mwamuzi msaidizi wa kwanza Mahmoud Ahmed Abo El Regal (Misri), Mwamuzi Msaidizi wa pili Samir Gamal Saad Mohamed (Misri), Mwamuzi wa akiba ni Ahmed Mahrous Elghandour (Misri), Kamishna wa mechi Salim Omary Singano (Tanga, Tanzania) na Mkaguzi wa waamuzi ni Alli Mohamed (Somalia).


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.