Kocha Mkuu wa Yanga Miloud Hamdi amesema amekiandaa kikosi chake kikamilifu kuhakikisha wanashinda mchezo dhidi ya Simba hapo kesho na kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya NBC
Akizungumza katika Mkutano na waandishi wa habari mapema leo, Hamdi alisema anatambua ugumu wa mchezo huo wa dabi ambao matokeo yake yataamua timu itakayokuwa bingwa wa ligi kuu msimu huu





