Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limeweka wazi ratiba ya michezo ya fainali za CHAN 2024, ambapo wenyeji Tanzania watafungua michuano hiyo kwa kuikabili Burkina Faso Uwanja wa Benjamim Mkapa Agosti 02, saa mbili usiku
Tanzania ipo Kundi B sambamba na timu za Burkina Faso, Madagascar, Mauritania pamoja na Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Nchi jirani ya Kenya itaanza mchezo wake wa kwanza wa Kundi A kwa kuikabili DR Congo Agosti 03, saa tisa alasiri.
Timu nyingine zilizopangwa Kundi A ni Zambia, Angola na Morocco. Wenyeji wengine wa fainali hizo Uganda watarusha karata yao ya kwanza kwa kuikabili Niger Agosti 04, saa mbili usiku.
Timu nyingine zilizopangwa Kundi C ni Afrika Kusini, Algeria na Guinea.
Jana Kocha Mkuu wa Stars Hemed Morocco alitangaza mjina ya wachezaji 27 ambao wataweka kambi Misri kujiandaa na michuano hiyo




