Klabu ya Azam Fc imetambulisha usajili wa beki wa kati Lameck Lawi aliyejiunga na timu hiyo kutoka klabu ya Coastal Union ya Tanga
Kulingana na taarifa iliyotolewa na Azam Fc jana, Lawi amesaini mkataba wa miaka miwili kuwatumikia wauza ice cream hao
Azam Fc imeshinda vita dhidi ya vigogo Simba na Yanga ambao kwa nyakati tofauti walihusishwa mchezaji huyo wa timu ya Taifa





