Kamati ya Uchaguzi ya TFF Imewang'oa wagombea watano wa nafasi ya Urais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na kubaki na jina moja la Wallace Karia anayetetea kiti hicho.
Akitangaza ripoti ya usahili wa uchaguzi huo Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa TFF Wakili Kiomoni Kibamba, amesema Karia ndiye mgombea pekee aliyekidhi vigezo na kwa mujibu wa Kanuni na kama kuna mtu anapingamizi bado ana nafasi ya kufanya hivyo
"Waliotia nia kugombea nafasi ya usais wa TFF walikuwa sita, mmoja hakuja kwenye usaili wakabaki watano, wanne wana mgogoro na kanuni na mgombea mmoja (Wallace Karia) yeye amekidhi vigezo vyote kwa hiyo yeye hakuwa na mgogoro na kanuni"
"Kwa upande wa waliotia nia kugombea ya ujumbe waliohudhuria zoezi la usaili ni watia nia 17, watia nia 10 wamekidhi vigezo vya awali vya kuingia kwenye uchaguzi wakisubiri mchato wa mapingizi"
"Wagombea saba waliobaki walikuwa na mgogoro na kanuni, maana yake hawakukidhi vigezo na masharti. Kama mtu hakuridhika na maamuzi ya kamati ya Uchaguzi ana haki ya kukata rufaa kwenye Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi ambayo ikifanya maamuzi inatuletea sisi ili tuendelee na mchakato,"alisema Kibamba



