Mshambuliaji wa timu ya taifa, Taifa Stars, Mbwana Samatta 'Samagol' amepata msiba mkuubwa wa kufiwa na baba mzazi, Ally Pazi Samatta.
Mzee Samatta amefariki dunia asubuhi ya leo Jumapili akiwa nyumbani kwake Mbagala Dar es Salaam na taarifa za kifo chake zimethibitishwa na mwanae, Mohamed Samatta.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa ndugu wa familia, Mzee Samatta alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya kiafya kwa hivi karibuni.
"Mzee amefariki leo nyumbani hakuwa ameugua kwa muda mrefu na juzi aliniambia njoo mwanangu unione daah! Ndio hivyo tena," amesema mmoja wa ndugu wa karibu wa familia hiyo.
Mzee Samatta enzi za uhai wake alikuwa mshambuliaji nyota aliyewahi kutamba na klabu kadhaa na kuichezea timu ya taifa, akivaa jezi namba 10 na alikuwa mtu mashuhuri katika jamii yake, akiheshimika kwa malezi bora aliyowapatia watoto wake, hasa Mbwana ambaye amekuwa nembo ya soka la Tanzania kimataifa.
Mwenye ez Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema, peponi AMEN..



