Klabu ya Azam Fc imethibitisha kukamilisha usajili wa aliyekuwa mlinda lango wa Simba Aishi Manula
Manula amesaini mkataba na Azam Fc ambao utamuweka Chamazi hadi mwaka 2028
Anatua Azam Fc baada ya kumaliza mkataba kunako klabu ya Simba aliyoitumikia tangu mwaka 2017
Manula ni kama amerejea nyumbani kwani alisajiliwa na Simba akitokea klabu hiyo mwaka 2017

Manula anakuwa usajili wa tatu kutangazwa na Azam Fc katika dirisha hili baada ya Muhsin Malima na Lameck Lawi




