Klabu ya Azam Fc imethibitisha kukamilisha usajili wa kiungo Himid Mao Mkami aliyekuwa mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba kunako klabu ya El Gaish ya Misri
Ni kama amerejea nyumbani kwani aliondoka nchini mwaka 2018 akiitokea Azam Fc na kujiunga klabu ya Petrojet ya Misri
Tangu wakati huo amecheza klabu kadhaa nchini Misri na hatimaye Azam Fc jana wakathibitisha kumsajili kwa mkataba wa mwaka mmoja kiungo huyo mwenye umri wa miaka 32 ambaye pia hucheza timu ya Taifa ya Tanzania
Himid anaungana na mlinda lango Aishi Manula ambaye ametambulishwa kurejea Azam Fc baada ya kuitumikia Simba kwa miaka nane





