International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu Julai 14 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 Jul 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu Julai 14 2025

Winga wa Manchester United Alejandro Garnacho amekataa kuhamia klabu ya Al Nassr, ya Saudia huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina mwenye umri wa miaka 21 akipendelea kuhamia Ulaya. (Telegraph)

Bayern Munich inatarajiwa kuelekeza mawazo yake kwa mshambuliaji wa Arsenal na Ubelgiji Leandro Trossard, 30, ikiwa haitafanikiwa kumsajili winga wa Liverpool Luis Diaz, 28. (Bild - kwa Kijerumani)

Mshambuliaji wa Brighton Evan Ferguson amekubali kuhamia Roma, huku klabu hiyo ya Italia ikiwa kwenye majadiliano kuhusu ada ya mshambuliaji huyo wa Jamhuri ya Ireland mwenye umri wa miaka 20. (Gianluca di Marzio - kwa Kiitaliano)

Nottingham Forest itakabiliana na ushindani kutoka kwa vilabu vya Ulaya kumsajili winga wa PSV Johan Bakayoko. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 ndiye alikuwa chaguo la kwanza kuchukua nafasi ya Anthony Elanga ambaye alisajiliwa na Newcastle wiki iliyopita. (Nottinghamshire Live)

Mawakala wa mshambuliaji wa RB Leipzig Benjamin Sesko, 22, wamewasiliana na Liverpool ili kutathmini nia yao ya kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Slovenia kufuatia uamuzi wa Arsenal kuelekeza nguvu zao kwa usajili wa Viktor Gyokeres wa Sporting Lisbon. (TBR Football)

Manchester United bado inamsaka mlinda lango lakini kipaumbele ya klabu hiyo ni kuimarisha kikosi chake, huku mchezaji wa kimataifa wa Cameroon Andre Onana, 29, akitarajiwa kuendelea kushikilia nafasi yake kama chaguo la kwanza. (i paper)

Everton imeungana na Roma katika mbio za kumsajili Neil El Aynaoui wa RC Lens licha ya kiungo huyo wa kati wa Morocco mwenye umri wa miaka 24 kufikia makubaliano ya awali na klabu hiyo ya Serie A. (Teamtalk)

Kipa wa Brest Marco Bizot, 34, anatarajiwa kujiunga na klabu ya Aston Villa na atasafiri hadi Uingereza kukamilisha mchakato huo. (L'Equipe - kwa Kifaransa)

Rangers iko mbioni kumsajili winga wa Crystal Palace Jesurun Rak-Sakyi, 22, kwa mkopo lakini inakabiliwa na ushindani kutoka kwa vilabu kadhaa. (Football Insider)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’