Kiungo wa klabu ya Singida Black Stars Arthur Bada amekamilisha uhamisho wake kwenda klabu ya JS Kabylie, imefahamika
Bada ametua Kabylie baada ya kuitumikia Singida BS kwa msimu mmoja akitokea Asec Mimosas ya Ivory Coast
Anajiunga na timu hiyo baada ya Kabylie kununua mkataba wake wa mwaka mmoja uliokuwa umebaki na Singida BS
Bada ambaye mapema msimu huu aliingia kwenye mijadala mikubwa baada ya kudaiwa kubadili uraia wake na kuwa Mtanzania, pia alikuwa akihusishwa na klabu ya Yanga
Hata hivyo ni wazi mpango wa kujiunga na Wananchi utakuwa umegonga mwamba..