Klabu ya Rayon Sports imethibitisha kuchuana na Yanga August 15 katika mchezo maalum wa kuadhimisha RAYON DAY. Mchezo huo umepangwa kupigwa katika uwanja wa Amahoro
Uongozi wa Rayon Sports ambao hivi karibuni ulikuwa nchini kuchota maarifa ya 'Transformation' kutoka kwa Yanga, wameanza matangazo ya mchezo huo

"Rayon Sports inayo furaha kutangaza kuwa tutacheza dhidi ya Yanga katika Siku ya Rayon Sports (Umunsi w'Igikundiro 2025)"
"Hii si mechi ya kirafiki tu, ni kama mechi ya hatua ya makundi! Hii ni KIPIMO GAME!," taarifa ya Rayon ilisomeka
Klabu ya Yanga inatarajiwa kuelekea Rwanda mapema August ambapo itaweka kambi ya muda mfupi ikiwa sehemu ya pre-season



