Timu ya taifa ya Kenya ‘Harambee Stars’, imejitoa katika mashindano maalum yaliyoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) ambayo yalitarajiwa kuanza hii leo kwenye Uwanja wa Black Rhino uliopo Karatu yakihususha timu nne.
Taarifa iliyotolewa Shirikisho la Kenya (KFK), imeeleza sababu ya kujiondoa katika michuano hiyo;
“Shirikisho la Soka la Kenya (FKF) linapenda kuutaarifu umma kwamba Harambee Stars imejiondoa kwenye Mashindano ya Mataifa Nne ya CECAFA nchini Tanzania.”
“Uamuzi huu umetolewa kufuatia mapendekezo na ushauri kutoka kwa benchi la ufundi la timu hiyo likiongozwa na Kocha Mkuu, Benni McCarthy baada ya kufanyiwa tathmini ya kina juu ya mazingira yaliyokuwapo ambayo yalionekana hayafai kwa ushiriki wa timu na maandalizi ya jumla.”
“Timu hiyo itarejea Kenya na kuendelea na maandalizi ya michuano ya Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) 2024, huku mkazo kamili ukielekezwa katika kuhakikisha kuwa wako tayari kwa kazi inayokuja.”




