Local,Normal News,

Harambee Stars yajitoa CECAFA 4

Joel JJ By Joel JJ
21 Jul 2025
Harambee Stars yajitoa CECAFA 4

Timu ya taifa ya Kenya ‘Harambee Stars’, imejitoa katika mashindano maalum yaliyoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) ambayo yalitarajiwa kuanza hii leo kwenye Uwanja wa Black Rhino uliopo Karatu yakihususha timu nne.

Taarifa iliyotolewa Shirikisho la Kenya (KFK), imeeleza sababu ya kujiondoa katika michuano hiyo;

“Shirikisho la Soka la Kenya (FKF) linapenda kuutaarifu umma kwamba Harambee Stars imejiondoa kwenye Mashindano ya Mataifa Nne ya CECAFA nchini Tanzania.”

“Uamuzi huu umetolewa kufuatia mapendekezo na ushauri kutoka kwa benchi la ufundi la timu hiyo likiongozwa na Kocha Mkuu, Benni McCarthy baada ya kufanyiwa tathmini ya kina juu ya mazingira yaliyokuwapo ambayo yalionekana hayafai kwa ushiriki wa timu na maandalizi ya jumla.”

“Timu hiyo itarejea Kenya na kuendelea na maandalizi ya michuano ya Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) 2024, huku mkazo kamili ukielekezwa katika kuhakikisha kuwa wako tayari kwa kazi inayokuja.”

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE →
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE →
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE →
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE →
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE →
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE →
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE →
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE →
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE →
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE →