Ni rasmi, klabu ya Yanga imethibitisha usajili wa kiungo mshambuliaji Offen Chikola
Chikola anajiunga na Yanga akitokea klabu ya Tabora United aliyon'gara msimu uliopita
Katika msimu uliopita, Chikola aliibuka kinara wa mabao katika kikosi cha Tabora United akifunga mabao nane
Mabao mawili aliyafunga katika mchezo dhidi ya Yanga, duru ya kwanza Tabora United ikiibuka na ushindi wa mabao 3-1 katika dimba la Azam Complex
Mwendelezo mzuri msimu mzima, akionyesha kiwango bora ni sababu ya Yanga kumsajili




