Chikola atambulishwa familia ya Wananchi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd July 2025


Chikola atambulishwa familia ya Wananchi

Ni rasmi, klabu ya Yanga imethibitisha usajili wa kiungo mshambuliaji Offen Chikola

Chikola anajiunga na Yanga akitokea klabu ya Tabora United aliyon'gara msimu uliopita

Katika msimu uliopita, Chikola aliibuka kinara wa mabao katika kikosi cha Tabora United akifunga mabao nane

Mabao mawili aliyafunga katika mchezo dhidi ya Yanga, duru ya kwanza Tabora United ikiibuka na ushindi wa mabao 3-1 katika dimba la Azam Complex

Mwendelezo mzuri msimu mzima, akionyesha kiwango bora ni sababu ya Yanga kumsajili


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.