Klabu ya Yanga imemtangaza Tshephang Mokaila kuwa kocha mpya wa viungo akichukua nafasi iliyoachwa na Taibi Lagrouni
Mokaila ni raia wa Afrika Kusini ambaye amewahi kufanya kazi katika klabu za Township Rollers, Marumo Gallants, Horoya Ac, Al Ahli Tripoli pia timu ya Taifa ya Botswana
Ujio wa Mokaila inaelezwa ni pendekezo la Kocha Mkuu wa Yanga Romain Folz ambaye analisuka upya benchi lake la ufundi
Mwishoni mwa wiki Yanga inatarajiwa kuanza kujifua Avic Town kujiandaa na mchezo dhidi ya Rayon Sports katika maadhimisho ya Rayon Sports Day, nchini Rwanda August 15



