Yanga yatambulisho kocha mpya wa viungo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 29th July 2025


Yanga yatambulisho kocha mpya wa viungo

Klabu ya Yanga imemtangaza Tshephang Mokaila kuwa kocha mpya wa viungo akichukua nafasi iliyoachwa na Taibi Lagrouni

Mokaila ni raia wa Afrika Kusini ambaye amewahi kufanya kazi katika klabu za Township Rollers, Marumo Gallants, Horoya Ac, Al Ahli Tripoli pia timu ya Taifa ya Botswana

Ujio wa Mokaila inaelezwa ni pendekezo la Kocha Mkuu wa Yanga Romain Folz ambaye analisuka upya benchi lake la ufundi

Mwishoni mwa wiki Yanga inatarajiwa kuanza kujifua Avic Town kujiandaa na mchezo dhidi ya Rayon Sports katika maadhimisho ya Rayon Sports Day, nchini Rwanda August 15


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.