Che Malone aagwa Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 30th July 2025


Che Malone aagwa Simba

Klabu ya Simba imemuaga aliyekuwa beki wake Che Malone Fondoh aliyejiunga na USM Algiers

Taarifa ya Simba imebainisha kuwa Che Malone amejiunga na USM Algiers baada ya makubaliano kati ya Simba na waajiri wake hao wapya

Beki huyo raia wa Cameroon alijiunga na Simba Julai 2023 akisaini mkataba wa miaka mitatu ambao ulipaswa kumalizika Juni 2026

Tayari Simba imemtangaza beki wa kati Rushine De Reuck kutoka klabu ya Mamelodi Sundowns kuwa mbadala wake


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.