Yanga, Simba ni jino kwa jino usajili

Joel JJ By Joel JJ • 2nd August 2025


Yanga, Simba ni jino kwa jino usajili

Miamba ya soka nchini Simba na Yanga inaendelea kushindana katika kutangaza wachezaji wapya ziliowasajili kwa msimu ujao wa mashindano mbalimbali.

Simba jana walitangaza usajili mpya wa mshambuliaji raia wa Ghana Jonathan Sowah, aliyejiunga na miamba hiyo akitokea Singida Blackl Stars, alikomaliza msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara akiwa na mabao 13 baada ya kusajiliwa dirisha dogo.

Muda mchache baadae, Yanga nayo ikatambulisha usajili wa Celestine Ecua raia wa Ivory Coast, aliyechezea Asec Mimosas ya Ivory Coast kwa mkopo akitokea Zoman FC.

Nyota huyo alikuwa Mchezaji Bora wa ligi wa Ivory Coast msimu wa mwaka 2024/25.

 


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.