Local,Normal News,

Samatta atua Ufaransa

Joel JJ By Joel JJ
5 Aug 2025
Samatta atua Ufaransa

Nyota wa soka wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta, amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuichezea Le Havre inayoshiriki Ligi Kuu Ufaransa (Ligue 1), hatua inayoweka historia kwa kuwa mchezaji wa kwanza Mtanzania kucheza katika ligi hiyo ya juu nchini humo.

Le Havre wamemtambulisha mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 32, wakithibitisha kuwa atavaa jezi namba 70 katika timu hiyo inayofahamika kama Sky & Navy. Uhamisho huo unakuja baada ya Samatta kuwa na mafanikio makubwa akianzia Afrika hadi kwenye baadhi ya ligi za Ulaya.

Kwa mujibu wa tovuti rasmi ya klabu hiyo, Samatta amesajiliwa kutokana na uzoefu, ubora wa kiufundi pamoja na uwezo wa kumalizia kwa ustadi.

“Nchini Tanzania, kuna hazina mbili kubwa zisizopingika: Mlima Kilimanjaro na Ally Samatta. Na wakati Le Havre si wageni wa kupanda milima mirefu, safari hii wameamua kuleta mlima wa vipaji moja kwa moja Normandy,” ilisomeka taarifa kwenye tovuti ya klabu.

Akiwa na jina la utani Samagoal kutokana na uwezo wake mkubwa wa kufumania nyavu, Samatta alijizolea umaarufu akiwa na TP Mazembe ya DR Congo ambako alishinda mataji manne ya ligi na kuisaidia timu hiyo kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa Afrika 2015.

Katika mwaka huohuo, alimaliza akiwa mfungaji bora wa mashindano hayo na kutangazwa kuwa Mchezaji Bora wa Afrika anayecheza barani humo.

Ufanisi wake Afrika ulimfungulia milango Ulaya akiianza safari yake katika timu ya Genk ya Ubelgiji na akiwa huko aliisaidia kutwaa taji la Ligi Kuu Ubelgiji na kujitokeza kuwa mmoja wa washambuliaji tishio zaidi katika ligi hiyo.

Uwezo wake ulimpa nafasi ya kujiunga na Aston Villa ya Ligi Kuu England kisha akacheza Fenerbahçe (Uturuki), Royal Antwerp (Ubelgiji) na kurejea kwa mara ya pili Genk.

Hivi karibuni, Samatta alikuwa akiitumikia PAOK Thessaloniki ya Ugiriki, ambako alicheza nafasi muhimu katika kuiwezesha timu hiyo kutwaa ubingwa wa Super League 2023–24.

Akiwa na Le Havre, Samatta anarajiwa kuleta si tu uzoefu, bali pia uwezo wa kuamua matokeo katika mechi.

Mwanaspoti

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
6h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
6h ago
READ MORE →
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
7h ago
READ MORE →
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
10h ago
READ MORE →
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
14h ago
READ MORE →
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
14h ago
READ MORE →
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
15h ago
READ MORE →
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE →
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
16h ago
READ MORE →
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
17h ago
READ MORE →