Kiungo mshambuliaji wa Simba Elie Mpanzu ameungana na wenzake Misri katika maandalizi ya msimu mpya wa mashindano 2025/26
Kuwasili kwa Mpanzu kunamaliza sintofahamu ya takribani wiki mbili na kuzima kabisa tetesi zilizokuwa zinadai mshambuliaji huyo yuko mbioni kuondoka Msimbazi
Mpanzu bado ni mali ya Simba kwa muda mrefu kwani mkataba wake wa miaka miwili ameutumikia miezi sita tu
Mcongomani huyo anatarajiwa kuwa mchezaji muhimu katika kikosi cha Simba kuelekea kukamilisha mipango yao msimu ujao



