Mpanzu aungana na Simba Misri

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th August 2025


Mpanzu aungana na Simba Misri

Kiungo mshambuliaji wa Simba Elie Mpanzu ameungana na wenzake Misri katika maandalizi ya msimu mpya wa mashindano 2025/26

Kuwasili kwa Mpanzu kunamaliza sintofahamu ya takribani wiki mbili na kuzima kabisa tetesi zilizokuwa zinadai mshambuliaji huyo yuko mbioni kuondoka Msimbazi

Mpanzu bado ni mali ya Simba kwa muda mrefu kwani mkataba wake wa miaka miwili ameutumikia miezi sita tu

Mcongomani huyo anatarajiwa kuwa mchezaji muhimu katika kikosi cha Simba kuelekea kukamilisha mipango yao msimu ujao


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.