Zimbwe Jr, Yanga yametimia

Joel JJ By Joel JJ β€’ 6th August 2025


Zimbwe Jr, Yanga yametimia

Majira ya saa 6 usiku Yanga ilimtambulisha beki wake mpya wa kushoto Mohamed Hussein 'Zimbwe Jr' aliyejiunga na tmu hiyo akitokea klabu ya Simba

Ilikuwa ni suala la muda, Yanga ilifanya 'umafya' kwa watani zao Simba kwa kumnyakua Zimbwe Jr wakati timu hiyo ikipambana kumuongezea mkataba

Zimbwe Jr ameondoka Simba baada ya kuitumikia timu hiyo kwa miaka 11, ameshinda mataji yote makubwa akiwa na Simba

Ni rasmi sasa anakwenda kufungua ukurasa mpya kunako klabu ya Yanga

Klabu ya Simba tayari imthibiti mlinzisha kumsajili beki wa kushoto Anthony Mligo kutoka klabu ya Namungo Fc

Mligo ametua Msimbazi kuziba nafasi iliyoachwa na zimbwe Jr


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.