Azam Fc yashusha msaidizi wa Ibenge

Joel JJ By Joel JJ β€’ 9th August 2025


Azam Fc yashusha msaidizi wa Ibenge

Klabu ya Azam Fc imamtambulisha Anicet Kiazayid kuwa Kocha Msaidizi wa timu hiyo inayonolewa na Kocha Mkuu Florent Ibenge

Kiazayid amerejea tena Ligi kuu ya NBC baada ya msimu uliopita kuiongoza Tabora United katika duru ya kwanza ambapo chini yake Tabora United ilikusanya alama nyingi ambazo pengine ndizo zilizowasaidia kumaliza katika nafasi ya tano kwenye msimamo

Kiazayid anaungana tena na Ibenge ambaye amewahi kufanya nae kazi kunako klabu ya AS Vita ya DR Congo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.