Klabu ya Azam Fc imamtambulisha Anicet Kiazayid kuwa Kocha Msaidizi wa timu hiyo inayonolewa na Kocha Mkuu Florent Ibenge
Kiazayid amerejea tena Ligi kuu ya NBC baada ya msimu uliopita kuiongoza Tabora United katika duru ya kwanza ambapo chini yake Tabora United ilikusanya alama nyingi ambazo pengine ndizo zilizowasaidia kumaliza katika nafasi ya tano kwenye msimamo
Kiazayid anaungana tena na Ibenge ambaye amewahi kufanya nae kazi kunako klabu ya AS Vita ya DR Congo




