Singida Black Stars itaanza kampeni ya Kombe la Shirikisho barani Afrika 2025/26, kwa kucheza na Rayon Sports ya Rwanda inayonolewa na kocha wa zamani wa Simba SC Robertinho.
Singida Black Stars itaanzia ugenini kisha itamalizia nyumbani Tanzania. Mshindi wa mechi ya Rayon Sports dhidi ya Singida Black Stars atakutana na mshindi wa mechi ya Flambeau Center ya Burundi dhidi ya mshiriki wa Libya (Libya 1).
Klabu ya Azam FC itaanza kampeni ya Kombe la Shirikisho barani Afrika 2025/26, kwa kucheza na Al Mereikh Bentiuya Sudan.
Azam FC itaanzia ugenini kisha itamalizia nyumbani Tanzania. Mshindi wa mechi ya Azam dhidi ya Al Mereikh Bentiu atakutana na mshindi wa mechi ya AS Port ya Djibout dhidi ya KMKM.



