International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne August 12 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
12 Aug 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne August 12 2025

Manchester City wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Real Madrid mwenye umri wa miaka 24 Rodrygo, ambaye thamani yake ni pauni milioni 87. (Fabrizio Romano)

Nottingham Forest wanakaribia kufikia makubaliano ya kumnunua kiungo wa kati wa Manchester City James McAtee, 22. (Subscription requires)

Chelsea na RB Leipzig wamemjadili mshambuliaji wa Ufaransa Christopher Nkunku, 27, wakati wa mazungumzo kuhusu mshambuliaji wa Uholanzi Xavi Simons, 22. (Talksport)

Mshambulizi wa Uswidi Alexander Isak, 25, atafikiria tu kujumuishwa tena Newcastle au kusaini mkataba mpya ikiwa Liverpool watamjulisha moja kwa moja kuwa mpango hauwezekani msimu huu wa joto. (Givemesport)

West Ham wanaandaa ofa ya kumnunua kiungo wa kati wa Southampton mwenye umri wa miaka 21 wa Ureno Mateus Fernandes, ambaye thamani yake ni pauni milioni 30. (Guardian)

Monaco wana nia ya kumsajili beki wa zamani wa Newcastle mwenye umri wa miaka 34 Kieran Trippier. (Sky Sports)

Inter Milan, Roma, Juventus na Napoli wameungana na AC Milan kuonyesha nia ya kutaka kumnunua Rasmus Hojlund, huku Manchester United wakiwa tayari kufikiria dau la Β£30m-Β£40m kwa mshambuliaji huyo wa Denmark mwenye umri wa miaka 22. (Subcription required)

Uhamisho wa mkopo wa kiungo wa kati wa Uingereza Jack Grealish kutoka Manchester City kwenda Everton unajumuisha chaguo la pauni milioni 50 kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 msimu ujao wa joto.(Subcription required)

Chelsea wametuma ofa ya pauni milioni 43 kwa beki wa kati wa Liverpool na Ufaransa Ibrahima Konate, 26 . (Defensa Central -in Spanish)

Newcastle pia wanavutiwa sana na kiungo wa kati wa Leicester City na Morocco Bilal El Khannouss, 21, lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa Leeds. (Telegraph)

Brentford na Newcastle wako kwenye mazungumzo ya kumsajili mshambuliaji wa Stade Rennais Mfaransa Arnaud Kalimuendo, huku The Bees wakiwa wamesonga mbele kidogo katika mazungumzo ya kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23. (L'Equipe - In French)

Everton wanavutiwa na winga wa Leicester Mghana Abdul Fatawu mwenye umri wa miaka 21 baada ya kushindwa katika ombi nyingi za kumnunua winga wa Southampton mwenye umri wa miaka 19 wa England aliye na umri wa chini ya miaka 21 Tyler Dibling. (Sky Sports)

Dominic Calvert-Lewin amemfuta kazi wakala wake alipokuwa akijaribu kutafuta klabu mpya. Mshambulizi huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 28 amefanya mazungumzo na Manchester United, Newcastle na Leeds. (Sport)

Chelsea wanafikiria kumnunua mlinzi wa Bayer Leverkusen na Ecuador Piero Hincapie, 23, kufuatia beki wa kati wa England mwenye umri wa miaka 22 Levi Colwill kuumia vibaya goti. (Caughtoffside)

Wolfsburg wanavutiwa na beki wa pembeni wa Sunderland wa Ireland Kaskazini Trai Hume, 23. (Sky Sports)

Kiungo wa kati wa Ujerumani Ilkay Gundogan, 34, ana nia ya kusalia Manchester City hadi mwisho wa dirisha la usajili la majira ya joto licha ya Galatasaray kumtaka. (Football Insider)

BBC

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’