Simba yagonga mwamba kwa Fei Toto

Joel JJ By Joel JJ β€’ 13th August 2025


Simba yagonga mwamba kwa Fei Toto

Jitihada za Simba kuinasa saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam Fc Feisal Salum 'Fei Toto' ni kama zimefika ukingoni baada ya mchezaji huyo kuamua kubaki Azam FC

Inaelezwa Fei Toto amekubali kuongeza mkataba wa mwaka mmoja kuendelea kuwatumikia matajiri hao wa Chamazi

Simba na Azam Fc zilikuwa katika majadiliano ya muda mrefu kupata suluhu ya uhamisho wa mchezaji huyo lakini ni kama Azam Fc wamefanikiwa kumshawishi asalie

Simba iliupa kipaumbele usajili wa Fei Toto ili kuboresha safu yake ya kiungo cha ushambuliaji lakini sasa baada ya mpango huo kukwana, ni wazi itaendelea kumtegemea Jean Charles Ahoua katika eneo hilo huku usajili mpya Morice Abraham akitarajiwa kuongeza nguvu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.