Jitihada za Simba kuinasa saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam Fc Feisal Salum 'Fei Toto' ni kama zimefika ukingoni baada ya mchezaji huyo kuamua kubaki Azam FC
Inaelezwa Fei Toto amekubali kuongeza mkataba wa mwaka mmoja kuendelea kuwatumikia matajiri hao wa Chamazi
Simba na Azam Fc zilikuwa katika majadiliano ya muda mrefu kupata suluhu ya uhamisho wa mchezaji huyo lakini ni kama Azam Fc wamefanikiwa kumshawishi asalie
Simba iliupa kipaumbele usajili wa Fei Toto ili kuboresha safu yake ya kiungo cha ushambuliaji lakini sasa baada ya mpango huo kukwana, ni wazi itaendelea kumtegemea Jean Charles Ahoua katika eneo hilo huku usajili mpya Morice Abraham akitarajiwa kuongeza nguvu



