Kocha Yanga ataka mechi zaidi za kirafiki

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd September 2025


Kocha Yanga ataka mechi zaidi za kirafiki

Kocha Mkuu wa Yanga Romain Folz amehitaji mechi zaidi za kirafiki kabla ya kikosi chake kutambulishwa kwenye kilele cha Wiki ya Mwananchi Septemba 12 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Baada ya wiki tatu za mazoezi ya kujenga utimamu wa mwili, kwa sasa Folz amejikita zaidi katika maandalizi ya kimbinu na ili kufanya tathmini ya kiasi gani wachezaji wake wameiva, ni kupitia mechi hizo za kirafiki

Mpaka sasa Yanga imecheza mechi nne za kirafiki katika kipindi hiki cha pre-season moja ikiwa ya ndani dhidi ya Yanga U20

Mechi nyingine tatu ilikuwa dhidi ya Rayon Sport, Fountain Gate na Tabora United ambazo zote Yanga ilishinda

Kesho Yanga inatarajiwa kujipima dhidi ya JKT Tanzania katika mwendelezo wa mechi hizo za kunoa silaha

Katika kilele cha wiki ya Mwananchi Yanga itaumana na Bandari Fc ya Kenya siku nne kabla ya mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya watani zao Simba ambao utapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa, Septemba 16


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.