Local,Normal News,Yanga

Kocha Yanga ataka mechi zaidi za kirafiki

Joel JJ By Joel JJ
β€’
3 Sep 2025
Kocha Yanga ataka mechi zaidi za kirafiki

Kocha Mkuu wa Yanga Romain Folz amehitaji mechi zaidi za kirafiki kabla ya kikosi chake kutambulishwa kwenye kilele cha Wiki ya Mwananchi Septemba 12 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Baada ya wiki tatu za mazoezi ya kujenga utimamu wa mwili, kwa sasa Folz amejikita zaidi katika maandalizi ya kimbinu na ili kufanya tathmini ya kiasi gani wachezaji wake wameiva, ni kupitia mechi hizo za kirafiki

Mpaka sasa Yanga imecheza mechi nne za kirafiki katika kipindi hiki cha pre-season moja ikiwa ya ndani dhidi ya Yanga U20

Mechi nyingine tatu ilikuwa dhidi ya Rayon Sport, Fountain Gate na Tabora United ambazo zote Yanga ilishinda

Kesho Yanga inatarajiwa kujipima dhidi ya JKT Tanzania katika mwendelezo wa mechi hizo za kunoa silaha

Katika kilele cha wiki ya Mwananchi Yanga itaumana na Bandari Fc ya Kenya siku nne kabla ya mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya watani zao Simba ambao utapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa, Septemba 16

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
8h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
14h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
15h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
17h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
20h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’