Leo Jumanne, Septemba 16, 2025, Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam utakuwa jukwaa la moja ya mechi kubwa zaidi barani, dabi ya Kariakoo kati ya Simba SC na Yanga SC, kuanzia saa 11 jioni.
Ni mchezo wa Ngao ya Jamii unaoashiria ufunguzi wa msimu mpya wa soka nchini, lakini zaidi ya hapo, ni vita ya heshima, historia na ubabe wa muda mrefu.



