International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu Septemba 22 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
22 Sep 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu Septemba 22 2025

Klabu ya Chelsea imefufua tena azma ya kumsajili kipa wa Ufaransa na AC Milan Mike Maignan, 30, na huenda ikamjumuisha kwenye orodha ya uhamisho katika dirisha lijalo la usajili wa wachezaji baada ya kipa wake wa sasa Mhispania Robert Sanchez, 27, kutofanya vizuri katika mechi yao dhidi ya Manchester United siku ya Jumamosi. (Daily Express)

Mkufunzi wa Brighton Fabian Hurzeler amemtaka kiungo Carlos Baleba kusalia licha ya tetesi kuibuka kwamba anandoka, huku Manchester United ikiwa na nia ya kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Cameroon mwenye umri wa miaka 21 msimu wa kiangaza. (Daily Mirror)

Everton wanafikiria kumsajili mchezaji huru Sergio Reguilon, 28, lakini beki huyo wa zamani wa Tottenham Hotspur anasemekana kupendelea kurejea katika nchi yake ya Uhispania. (Football Insider)

Klabu za ligi kuu ya England kama vile Liverpool, Manchester United na Chelsea zina nia ya kumsajili beki wa Juventus na Brazil Gleison Bremer, 28. (Team Talk)

Crystal Palace hawana mpango wa kumuuza kiungo wa kati wa Uingereza Adam Wharton, 21, katika dirisha la uhamisho la Januari, huku Liverpool na Real Madrid zikiwania saini yake. (Football Insider)

Beki wa Bayern Munich Mfaransa Dayot Upamecano, 26, anataka kuhamia Real Madrid mkataba wake utakapokamilika msimu ujao. (Marca - kwa Kihispania)

Tottenham Hotspur ina nia ya kubadilisha mkataba wa mkopo wa kiungo wa kati wa Ureno Joao Palhinha, 30 kutoka Bayern Munich kuwa wa kudumu mwezi Januari. (TBR Football)

BBC

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
4m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
33m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’