International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi Januari 22 2026

Joel JJ By Joel JJ
β€’
22 Jan 2026
Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi Januari 22 2026

Kiungo wa AC Milan na England Ruben Loftus-Cheek, 29, analengwa na Aston Villa, ambayo inataka kuimarisha safu yake ya kati baada ya mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa Boubacar Kamara, 26, kupata jeraha baya la goti. (Telegraph - usajili unahitajika)

Loftus-Cheek pia ametolewa kwa Manchester United, na mazungumzo ya awali yamefanyika. (Talksport)

Villa imemuulizia mshambuliaji wa Fenerbahce Youssef En-Nesyri katika muda wa saa 24 zilizopita, lakini mchezaji huyo wa Morocco, 28, ataamua mustakabali wake hivi karibuni huku Napoli na Juventus pia zikimtaka. (Fabrizio Romano)

Tottenham iko tayari kutoa pauni milioni 25 kumsajili winga wa West Ham Mholanzi Crysencio Summerville, 24. (Mail)

Liverpool inavutiwa na beki wa Tottenham na Uholanzi Micky van de Ven, 24, ambaye bado hajasaini mkataba mpya na Spurs. (Mail - usajili unahitajika)

Manchester United inataka kusalia na kiungo wa Ureno Bruno Fernandes, 31, kwa mwaka mwingine na wangependa kujua msimamo wake kabla ya Kombe la Dunia msimu huu. (ESPN)

Nottingham Forest itamruhusu beki wa Brazil Cuiabano, 22, kuondoka kwa mkopo mwezi huu, huku beki wa pembeni wa Liverpool, 29, Ugiriki, Kostas Tsimikas, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Roma,akiwa miongoni mwa wanaolengwa. (Athletic - usajili unahitajika)

Ombi la Forest kumsajili mlinzi wa Napoli Mathias Olivera limekataliwa, lakini bado ipo kwenye mazungumzo na mchezaji huyo wa kimataifa wa Uruguay, 28. (Tuttomercatoweb - kwa Kiitaliano)

Celta Vigo wamewasilisha ombi rasmi kwa Wolves kumsajili kwa mkopo Fer Lopez, 21, na itagharamia mshahara wote wa kiungo huyo mshambuliaji wa Uhispania aliye na umri wa chini ya miaka 21. (Sky Sports)

BBC

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’